Pages

Welcome to GLOBAL EDUCATION LINK. STUDY ABROAD through US. WE Admit YOU to Overseas Universities, We give YOU right Information, WE Advice on Course Selection, WE Guide YOU On Your CAREER, WE Guide YOU on University SELECTION, WE Assist YOU on YOUR Visa Process. JOIN US NOW OR CALL US ON 0656 200 200 for MORE Information. WELCOME TO FEEL THE DIFFERENCE.

MATUKIO YANAYOTOKEA HIVI SASA KWENYE UCHAGUZI WA KENYA


 Wapiga kura  katika mtaa wa Kibera.

 Foleni za wapiga kura Mombasa.

 Foleni za wapiga kura Nairobi.

Raia wa Kenya wameanza shughuli ya kupiga kura katika uchaguzi wa kwanza unaofanyika chini ya katiba mpya.

Katika uchaguzi huu watamchagua rais pamoja na wawakilishi wa wanawake, magavana, na maseneta wa majimbo 47 ya nchi hiyo.
Katika mji mkuu Nairobi misururu mirefu ya wapigakura ilionekana kabla ya vituo vya kupigia kura kufunguliwa 12 za Afrika mashariki.
Ushindani mkubwa wa kiti cha urais unatarajiwa kuwa baina ya kiongozi wa muungano wa Cord, Raila Odinga, na yule wa muungano wa Jubilee, Uhuru Kenyatta.

Japokuwa tume ya uchaguzi IEBC inawakubalia watu wawasindikize wazee au wagonjwa kupiga kura, wapigaji kura wengine wanawakataza kufanya hivyo.



Waziri mkuu Raila Odinga ambaye pia anagombea urais amepiga kura yake katika eneo la Kibera. Amesema licha ya kupata habari za baadhi ya vituo vya kupigia kura kuwa na hitilafu kidogo, wapiga kura wasiwe na wasiwasi kwani mambo yatakuwa shwari

Share