Kiwango cha udahili  wa wanafunzi wa kike  kujiunga na elimu ya 
vyuo vya  juu kimeongezeka kutoka wanafunzi 49,959 mwaka 2010/11 hadi 
60,592 (asilimia 19).
Aidha,  katika shule za sekondari umeongezeka kutoka wanafunzi 
728,528 hadi 802,554 ikiwa (asilima 9.2) ukiwa ni uwiano wa wanafunzi wa
 kike na wa kiume kuwa asilimia 44.8.
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu,
 alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa wakati akizumgumzia maadhimisho 
ya siku ya wanawake duniani leo.
Alisema vitendo vya ukatili kama ukeketaji vimepungua kutoka 
asilimia 18 hadi asilimia 15 kwa mwaka 2010 wanatarajia kiwango hicho 
kitapungua zaidi ifikapo mwaka 2015.
Mwalimu alisema  wanawake wamewezeshwa kiuchumi kwa kuwapatia elimu
 ya ujasiriamali na mikopo yenye masharti nafuu kupitia benki ya 
wanawake Tanzania hadi kufikia Juni 2012 ilitoa mikopo yenye thamani ya 
Sh. bilioni 1.2 kwa wanawake 5,270 na wanaume1,157.
 
Kauli mbiu ya mwaka huu ni ‘Uelewa wa masuala  ya jinsia katika jamii,ongeza kasi’
 
.jpg)